Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Hawza, je, unatafuta njia ya kuongeza mapenzi ya Mwenyezi Mungu ndani ya moyo wako? Ayatullah Bahjat anaeleza kuwa "kumswalia Mtume kwa mapenzi" ndiyo ufunguo wa mafungamano haya. Kwa kumswalia Mtume, unajenga mafungamano ya kina zaidi na Mola wako Mpendwa.
Maneno ya Ayatullah Bahjat - Quddisa Sirruh:
“Mtu anayetaka urafiki na mapenzi yake yazidi, katika nyiradi, adaab na ibada mbalimbali, hakuna jambo lililo rahisi zaidi kuliko kusoma kumswalia Mtume mara nyingi zaidi;
Mtu atakapo mswalia Mtume kwa moyo wa mapenzi, ataelewa namna mapenzi yake yanavyozidi kwake; lakini kwa sharti la kuwa na imani sahihi, yaani, atambue kwamba dhikri hiyo inamvuta kumuelekeza kwa Mola wake na Mpenzi wake wa kweli.”
Maoni yako